Wanajeshi wa Chad wako nchini Nigeria kupambana na Boko Haram
Kumekuwa na mapigano makali kati ya
Vikosi vya Chad na Wanamgambo wa Boko Haram kaskazini mashariki mwa
Nigeria.Msemaji wa Jeshi la Chad amesema vikosi vyake ambavyo ni sehemu
jeshi la kimataifa wamepambana na Boko Haram mjini Gamboru, katika eneo
la mpaka wa Nigeria na Cameroon.
Taarifa zinasema Wanajeshi tisa
wa Chad na takriban wanamgambo wa Boko Haram 200 wameuawa, lakini idadi
ya wanamgambo wanaodaiwa kuuawa haijathibitishwa.Boko haram wamekuwa wakipambana na Vikosi vya Cameroon upande wa pili wa Mpaka, mjini Fotokol nchini humo.
CHANZO BBC
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni