Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Jumatano, 4 Februari 2015

WANAJESHI WA CHAD WAINGIA NIGERIA



Kikosi cha kijeshi cha Nigeria 
Vikosi vya Chad vimeingia nchini Nigeria kuongeza nguvu katika mapambano dhidi ya Wanamgambo wa kiislamu, Boko Haram.
Msemaji wa idara ya usalama nchini Nigeria Mike Omeri amesema mapigano yalilenga eneo la kaskazini mashariki mwa mji wa Gamboru.
Kuingia kwa jeshi la Chad kunaelezwa kuwa sababu mgogoro na Boko Haram umefikia hatua ya kutoka nje ya mipaka ya Nigeria na kuathiri ukanda mzima.
Juma lililopita, Vikosi vya Chad viliripotiwa kuingia mjini Malumfatori, mji ulio karibu na mpaka kati ya Chad na Niger, baada ya mapambano dhidi ya Wanamgambo.
Kiongozi wa kundi la Boko Haram, Aboubakar Shekau ametishia kuanzisha matawi ya wanamgambo katika maeneo mengine nchini Nigeria,Niger,Chad na Cameroon.
Umoja wa Afrika una mpango wa kuunda kikosi cha Wanajeshi 7,500 kupambana na Boko Haram.
CHANZO BBC

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni