Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Jumanne, 31 Machi 2015

HABARI YA HIVI PUNDE;-AJALI ILIYO SABABISHA KIFO CHA MSANII MAARUFU.


LEO NI SIKU YA WAJINGA NDUGU YANGU...........
MC.RAY
0659/375263

ENDELEA KUTIZAMA PICHA ZILIZO JAA UCHESHI KUPITIA BLOGS YKO YA rayshughuli.blogspot.com.

CHEZEA KUBET WEWE,,,,,,

MC,RAY
0659/375263

FACEBOOK KUFUNGUA HUDUMA MPYA.


Mtandao wa facebook umethibitisha kwamba unafungua huduma yake ya messenger kwa wajenzi .Habari hizo zilitangazwa na Mark Zuckerberg katika kongamano la nane la wajenzi lililofanyika mjini San Fransisco.Zaidi ya programmu 40 mpya zikiwemo habari za hali ya anga tayari zimeandaliwa kwa huduma hiyo.Mtandao huo wa kijamii pia ulionyesha programu yake ya video inayomruhusu mtumiaji kusukuma kamera huku kanda hiyo ikicheza.
CHANZO BBC.

WAZAZI WANAPASWA KUDHIBITI UNENE WA WATOTO WAO.


Sheria madhubuti zinapaswa kutungwa ilikuzima matangazo ya kufana ya vyakula vyenye mafuta mengi.
Madaktari wanasema kuwa wazazi wengi hawajui madhara ya afya kwa watoto walionenepa kupita kiasi.
Katika utafiti huo uliowajumuisha zaidi ya familia 2,976 nchini Uingereza ni wazazi 4 pekee waliokuwa na shauku kuwa mtoto wao alikuwa amenenepa kupita kiasi.
Madaktari wenye walikuwa wamewatambua watoto 369 kati yao waliokuwa na kiwango cha juu cha mafuta mwilini.
Takwimu hizo zinaonesha kuwa watoto walionenepa kupita kiasi sasa wamekuwa kawaida tu majumbani.
Watafiti hao wanaonya kuwa hili ni janga kwa afya ya jamii.

Asilimia 31% ya wazazi hawajui kutambua dalili za mtoto aliyenenepa kupita kiasi
Aidha utafiti huo ulielezea kuwa takriban mtoto mmoja kati ya watano ambao wanaumri wa miaka 6 tayari wanauzito unaozidi kadri kwa asilimia 14%.
Kundi hilo la watafiti kutoka taasisi ya usafi ya Uingereza ''London School of Hygiene and Tropical Medicine'' lilizitembela familia 3,000 na kuwahoji iwapo watoto wao walikuwa ni wanene kupita kiasi wastani ama webamba?
majibu yao yaliwaduwaza.
Takriban thuluthi moja 31% ya wazazi walidunisha uzani wa watoto wao.
Proffesa Russell Viner, wa chuo cha Afya ya Watoto aliiambia BBC kuwa wazazi wa kisasa wanamajukumu wengi na hivyo watoto wao hutunzwa na vijakazi asilimia kubwa ya muda ambao wazazi wako makazini mwao.

Sheria madhubuti zinapaswa kutungwa ilikuzima matangazo ya kufana ya vyakula vyenye mafuta mengi.
''Hili ni janga ambalo linatokota ,madhara yake yataonekana siku za usoni katika njia ya maradhi mengi tu yanayohusiani na unene'' alisema Professa Viner.
Kwa mujibu wa Dakta Dame Sally Davies, ''Afya ya watoto kwa sasa imehujumiwa na dhana kuwa japo mtu ni mnene jamii haitambagua kwani watu wengi duniani ni wanene''
"Nafikiri kwamba itatubidi tuwaelimishe wazazi kuhusiana na maswala ya afya ya watoto wao na pia kuwaeleza kuwa wanapaswa kufuatilia kwa karibu unene au sio wa watoto wao''
CHANZO BBC.

OBAMA KUZURU KENYA JULAI.


Obama kuzuru Kenya Julai 
Ikulu ya Marekani imetangaza kuwa, Rais Barrack Obama atazuru Kenya mwezi Julai mwaka huu, taifa alikozaliwa babake.
Inasemekana kuwa Bwana Obama, atahudhuria mkutano mkubwa wa kimataifa kuhusu ujasirimali, utakaofanyika katika mji mkuu wa nchi hiyo-Nairobi.
Tangu awe Rais wa Marekani, Barack Obama hajawahi kuzuru taifa hilo la Afrika Mashariki kama Rais.

Obama, atahudhuria mkutano mkubwa wa kimataifa kuhusu ujasirimali
Alizuru mataifa kadhaa za Afrika ikiwemo ziara ya taifa jirani Tanzania mnamo mwaka 2013 bila kuzuru Kenya.
Alizuru Kenya akiwa seneta mnamo mwaka 2006.
Bababke Obama alisomea Marekani na hatimaye kurejea Kenya baada ya Obama kuzaliwa.
chanzo bbc.

HABARI ZA HIVI PUNDE;JENERALI BUHARI NDIYE RAIS MPYA NIERIA

Rais mpya wa Nigeria Buhari
Muhammadu Buhari, ni Muisilamu, mzaliwa wa Jimbo la Katsina, Nigeria kaskazini.
Alizaliwa mwaka 1942, Buhari alikuwa kiongozi wa saba wa taifa la Nigeria, baina ya mwaka 1983-1985.
Ni jenerali mstaafu aliyepata mafunzo ya kijeshi katika Nigeria, Uingereza, India, na Marekani.
Na aliwahi pia kushika nyadhifa za ugavana, kamishna wa raslimali ya mafuta, mwenyekiti wa shirika la umma la mafuta, na pia mwenyekiti wa Mfuko wa Amana ya Mafuta.

Wafuasi wa rais Buhari wakishangilia ushindi huo
Licha ya kushindwa mara katika chaguzi tatu, amerejea kushindania tena urais, dhidi ya rais alo-madarakani Goodluck Jonathan,
Mkristo, anaye toka eneo la Niger Delta, kusini Nigeria, kwa mara ya pili, katika uchaguzi wa Machi. Unaonesha kuwa mchuano mkali.
Kuambatana na mandhari ya kisiasa, Buhari si limbukeni. Kushindwa mwaka 2003 na tena 2007, alitambia matokeo ya chaguzi hizo mahakamani bila mafanikio.

Buhari alimshinda rais anayeondoka Goodluck Jonathan katika uchaguzi ulioshuhudia ushindani mkubwa
Ingawaje, Buhari anazingatiwa kuwa kiongozi mwenye ufuasi mkubwa na heshima nyumbani, hususan katika rubaa za kaskazini Nigeria.
Na hii inatokana na sera zake za kupambana na ufisadi na ukosefu wa nidhamu, wakati alipokuwa mtawala wa kijeshi.

Mabango ya Uchaguzi
Kimataifa, Buhari pia anasemekana kuheshimiwa.
Yajulikana kwamba ni yeye na marehemu Nelson Mandela tu ndio Wafrika binafsi waloalikwa na Ikulu ya White House, Marekani, kuhudhuria sherehe za kutawazwa Barack Obama.
Kampeni ya Jenerali Buhari, ilitilia mkazo mambo kadha, miongoni mwake utawala bora, kufufua uchumi, maendeleo ya miundombinu,
umeme na nishati, kilimo, elimu, afya, ardhi na usafiri, kuwezeshwa wanawake, usalama, na ajira. Ingawaje, uwili wa nafsi yake bado unazusha masuala, je ni wa kijeshi au kidemomkrasi?
CHANZO  BBC.

VIONGOZI 175 WALIOTUHUMIWA KWA UFISADI WATAJWA.


Majina ya maafisa wakuu wa serikali wanaotuhumiwa kuhusika na ufisadi yamewasilishwa katika mabunge Kenya chini 
Orodha ya majina ya maafisa wakuu wa serikali wanaotuhumiwa kuhusika na ufisadi imewasilishwa katika mabunge mawili 
nchini Kenya huku kukiwa na mjadala mkali kuhusu jinsi orodha hiyo ilivyowasilishwa bungeni.
Kikao cha bunge la senate lilisitishwa kwa muda kuruhusu wabunge kusoma ripoti hiyo.
Katika bunge la taifa wabunge nao walitaka kuzima mjadala kuhusiana na ripoti hiyo iliyowasilisha na raia kwa misingi ya kukiuka sheria.
Robert Kiptoo ana maelezo zaidi kutoka Nairobi.
Orodha hiyo ina majina 175 ya maafisa wakuu serikalini wakiwemo mawaziri, makatibu wa wizara na maafisa wengine wa taasisi za umma na hata za kibinfasi.

Maafisa hao wa serikali sasa wameshurutishwa kungatuka madarakani
Maafisa hao wa serikali sasa wameshurutishwa kungatuka madarakani kwa muda wa siku sitini ili kuruhusu uchunguzi wa kina.
Orodha hiyo ambayo wakenya wakisubiri kwa kwa hamu na ghamu hatimaye ilijadiliwa katika mabunge yote licha ya upinzani kutoka kwa wabunge kadhaa.
Mjadala mkali uliibuka katika mabunge hayo hadi spika wa bunge la senate kusitisha kikao kwa muda kuruhusu masenate kusoma ripoti hiyo ya rais.
Hata hivyo mjadala ulipoanza wabunge wengi wanaoegemea upande wa serikali waliunga mkono wakisema vita dhidi ya ufisadi ni sharti viimarishwe.
wabunge wa upinzani nao wakijaribu kupinga mjadala huo, wakidai kuwa sheria haikufuatwa na rais alipowasilisha ripoti hiyo.

Wabunge wa upinzani wanajaribu kupinga mjadala huo
Aidha wamesema kuwa ripotio haina sahihi kama inavyohitajika.
Mpinzani mkuu wa rais Kenyatta na kiongozi wa upinzai, Raila Odinga, akiongea baada ya kuwasili nchini kenya kutoka uchina siku ya jumapili,
alisema hatua hiyo ya rais ni sawa na ulaghahi dhidi ya wakenya.
Amesema kutoka na jinsi mfumo wa mahakama upo, ni vigumu sana kwa uchunguzi dhidi ya maafisa 175 kukamilishwa kwa siku sitini ikizingatiwa
kuwa kuna baadhi ya kesi za ufisadi ambazo zimesalia mahakamani kwa zaidi ya miaka kumi.
chanzo bbc.

ALIYE WAUA WAINGEREZA WAWILI KUNYONGWA.


Kitanzi cha kunyongea watu
Mahakama ya Malaysia imemkuta na hatia ya mauaji mtu mmoja kwa tuhuma za mauaji ya wanafunzi wawili wa udaktari kutoka nchini Uingereza.Mauaji hayo yanadaiwa kufanyika August mwakajana katika kisiwa cha Borneo.
Jaji wa mahakama hiyo amesema mahakama imeidhishwa na ushahidi dhidi ya mshitakiwa na kuona anastahili adhabu. Hukumu hiyo inayomkabili Zulkipli Abdullah anadaiwa kuwaua Neil Dalton na Aidan Brunger.
Kwa mjibu wa hukumu hiyo ya mauaji, Abbdullah atanyongwa hadi kufa.
CHANZO BBC.

MWENDESHA MASHITAKA AUAWA UGANDA

Askari akikagua gari ambalo lilikuwa likiendeshwa na Joan Kagezi 
Watu wenye silaha wamemuua mwendesha mashitaka mkuu katika kesi ya watuhumiwa wa Kiislam wanaotuhumiwa kuua watu kadha katika mashambulio ya bomu mwaka 2010.
Mwendesha mashitaka huyo Joan Kagezi ambaye alikuwa kaimu mkurugenzi mwendesha mashitaka msaidizi nchini Uganda ameuawa kwa kupigwa risasi na watu waliokuwa katika pikipiki wakati akiendesha gari kurudi nyumbani mjini Kampala.
Kesi inayoendelea inawahusu watu kumi na watatu wanaotuhumiwa kuwa wapiganaji wa kikundi cha al-Shabaab.
Wanatuhumiwa kuua watu zaidi ya sabini wakati wakiangalia Fainali za Kombe la Dunia za mwaka 2010 katika mgahawa mmoja na katika uwanja wa klabu ya rugby.
Wiki iliyopita Marekani ilisema ilipata "habari za kuwepo uwezekano wa shambulio" katika maeneo ya mji ambayo raia wa mataifa ya magharibi wanakutana.
Serikali ya Uganda imesema Marekani ilionya juu ya uwezekano wa kuwepo kwa mtu anayejitoa mhanga akijaribu kuingia nchini humo.
Msemaji wa serikali amesema Uganda ilikuwa katika kitisho kwa sababu imechangia askari wengi katika jeshi la Umoja wa Afrika linalolinda amani nchini Somalia wakipambana na kundi la al-Shabab ndani ya Somalia.
CHANZO BBC.

MTANZANIA AKAMATWA KWA UGAIDI KENYA.

Ummul-Khayr Sadir Abdul (19).
Vyombo vya usalama nchini Kenya, vinawashikilia wasichana watatu akiwamo Mtanzania, kwa kile kunachodaiwa kutaka kujiunga na kundi la kigaidi la al-Shabaab huko Somalia.
Taarifa kutoka kwa Kamishna wa Polisi Jimbo la El -Wak, mpakani mwa Kenya na Somalia, Nelson Marwa amesema Mtanzania aliyekamatwa, alijieleza kuwa ni mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Kimataifa cha Afrika, Sudan.
Mtanzania huyo, Ummul-Khayr Sadir Abdul (19), mwenyeji wa Zanzibar, anatajwa kuwa kiongozi wa kundi hilo lililopanga kujiunga na al-Shabaab.
Wasichana wengine waliokamatwa pamoja na Ummul-Khayr, ni Maryam Said Aboud na Khadija Abubakar Abdulkadir wote raia wa Kenya.
“Hawa wasichana watatu, inaaminika kuwa walikuwa wanakwenda Somalia kupata mafunzo ya kigaidi na baadaye kufanya mashambulizi ya kujitoa mhanga,” alisema Kamishna Marwa.
Akizungumzia suala hilo, Kaimu Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai, DCI Diwani Athumani alisema: “Tunafuatilia hatujapokea taarifa zaidi ya hizo.”
Kamishna Marwa alisema raia hao wawili wa Kenya, mmoja ni mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Mount Kenya kilichopo Thika, Jimbo Kiambu na mwingine ni mwanafunzi wa Sekondari ya Burhania, iliyopo Malindi, Kilifi.
“Serikali imepata taarifa kuhusu watu wanaokusanya watu kutoka Afrika Mashariki ili wakajiunge na makundi ya ugaidi nchini Somalia, wakala wetu wa usalama wamepata taarifa hizo na kufanikisha kukamatwa kwa wasichana hao,” alisema Kamishana Marwa.
Hivi karibuni, tovuti ya al-Jazeera ilitoa taarifa za kukamatwa kwa mkanda wa video ulioonyesha mwakilishi wa kundi la kigaidi la Dola ya Kiislamu ya Iraq na Levant (ISIL) akimtaka kiongozi wa kundi la al-Shabaab kuliimarisha kwa kufanya mashambulizi ya kigaidi katika miji ya Mwanza na Dar es Salaam.
Kamishna Marwa alisema ingawa nyaraka za wasichana hao zote zinaonyesha kuwa ni wanafunzi, lakini bado walibanwa kwa maswali kuhusu sababu inayowapeleka nchini Somalia.
Aliongeza zaidi kuwa chanzo cha habari cha kiusalama kilieleza kuwa nyaraka za wasichana hao zilionyesha kuwa walikuwa wakienda kuolewa na wanajeshi wa kundi la al-Shabaab.
chanzo bbc.

HABARI ZA HIVI PUNDE;BUHARI ANUSIA USHINDI WA URAIS NIGERIA.

Jenerali Muhammadu Buhari anaongoza kwa zaidi ya kura milioni mbili zaidi ya mpinzani wake wa karibu ambaye ni rais Goodluck Jonathan
Huku yakisalia majimbo machache, Buhari anaongoza kwa karibu kura milioni tatu mbele ya Rais wa sasa Goodluck Jonathan.
Awali kulikua na matukio ya kurushiana maneno katika ukumbi mkuu wa hesabu ya kura pale mwakilishi wa chama tawala-PDP Elder Orubebe alipolalamikia tume ya uchaguzi kwa kupendelea.
Kumekua na kurushiana cheche za maneno makali katika ukumbi mkuu wa kuhesabu kura nchini Nigeria.
Mwakilishi wa chama tawala PDP-Elder Orubebe, alivuruga shughuli ya kutangazwa matokeo ya kura akidai tume ya uchaguzi ilikua ikipendelea upande mmoja.
 
Mawakala wa wagombeaji wakuu
Mwenyekiti wa tume ya kitaifa ya uchaguzi mkuu Nchini Nigeria, Attahiru Jega, alimuonya Elder Orubebe kuwa mwaangalifu kutokana na matamshi yake hayo aliyotoa.
Mwandishi wa BBC aliyeko ukumbi huo mjini Abuja anasema huenda vurugu hizo ni ishara kuwa, PDP inahisi kushindwa.
Huku majimbo mengi yakitoa matokeo yake mgombea wa upinzani, Muhammadu Buhari wa chama cha APC, anaendelea kuongoza kwa wingi wa kura, huku akifuatiwa na Rais Goodluck Jonathan.
Generali Buhari wa chama cha All Progressives Congress (APC) anaonekana kusajili matokeo mema mapema hata kabla ya kuhesabiwa kwa kura za mjini Lagos.
Matokeo ya uchaguzi mkuu nchini Nigeria yanatarajiwa kutangazwa saa chache zinazokuja wakati
majimbo yaliyosalia yakisubiriwa kutangaza matokeo yao.

Tume ya uchaguzi imesema itaendelea kutangaza matokeo ya uchaguzi Jumanne
Mwandishi wa BBC mjini Abuja amesema mchuano bado ni mkali.
CHANZO BBC.

Ijumaa, 27 Machi 2015

BRAZILI YAICHAPA UFARANSA 3-1.

Timu ya Taifa ya Brazil
Brazili jana aliikimbiza mchamchaka Ufaransa baada ya kuichabanga magoli matatu kwa moja.
Haikuwasaidia Ufaransa kuanza kuona lango la Brazil katika dakika ya 21 kwa goli lililofungwa na Raphael Varane kwani ni kama waliichokoza kundi la nyuki kwani goli hilo lilirudishwa na Oscar dos Santos Emboaba Júnior katika dakika ya 40, na hatimaye kushindiliwa magoli mengine mawili kupitia kwa Neymar da Silva Santos, Júnior, na Luiz Gustavo na hivyo hadi mechi hiyo inamalizika Brazil 3 Ufaransa 1.
Katika mechi nyingine za kimataifa za kirafiki zilizochezwa hapo jana, Bahrain iligeuzuwa chapati na Colombia pale waliposhindiliwa magoli 6 kwa mtungi huku Iran ikiwapa darasa Chile kwa kuichabanga magoli mawili kwa nunge.
Leo kutakuwa na mechi moja ya kimataifa ya kirafiki ambapo Canada watairibisha Guatemala
CHANZO BBC.

JOHN TERRY AONGEZEWA MKATABA CHELSEA.

Nahodha wa Chelsea John Terry aongezewa mkataba 
Nahodha wa kilabu ya Chelsea John Terry ameongeza mkataba wake katika kilabu hiyo hadi mwisho wa msimu wa mwaka 2015-16.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 34,ambaye mkataba wake wa awali unakamilika mwisho wa msimu huu ameichezea Chelsea mara 550.
Chelsea wanaongoza kwa pointi sita katika jedwali la ligi ya Uingereza wakiwa na mechi moja zaidi ambayo hawajacheza dhidi ya wapinzani wao na mkufunzi Jose Mourinho anasema kuwa kandarasi hiyo ya mwaka mmoja si ya kumpatia asante John Terry bali ni kwa sababu anaendelea kucheza vizuri.
Ni mlinzi wa kiwango cha juu.
Mourinho hivi majuzi alisema kuwa ana hakika kwamba Terry atapewa mkataba mpya,ikiwa ni miongoni mwa sera za kilabu hiyo kuwaongezea kandarasi awchezaji ambao wamepitisha umri wa miaka 30.
CHANZO BBC.

WALCOT ASEMA HAJAKOSANA NA WENGER.

Theo walcot
Mshambuliaji wa Arsenal Theo Walcot anasema kuwa hajakosana na meneja Arsene Wenger na kuongezea kwamba bado hajaanza mazungumzo ya mkataba mpya na kilabu hiyo.
Mkataba wa Walcot unakamilika mwaka 2016 na Wenger amesema kuwa anatarajia kuwa na mda mrefu wa makubaliano.
''Ripoti zinazosema nimekosana na kocha juu ya kandarasi ni upuzi mtupu'',alisema mchezaji huyo wa miaka 26.
Hatujaanza mazungumzo yoyote juu ya kandarasi yangu na lengo langu kuu ni kufanya vyema katika kilabu hii.
CHANZO BBC.

MATUMLA KUVAANA NA WANG XIN HUA.

Mabondia Xin Hua wa China na Mohamed Matumla wa Tanzania wakitambiana kabla ya pambano lao la Ijumaa 
Bondia Mohamed Matumla wa Tanzania atapanda ulingoni Ijumaa kutwangana na Wang Xin Hua wa China.
Mchezo huu ni wa uzito wa super bantam kuwania nafasi ya kugombea taji la dunia la WBF utakaofanyika katika ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es salaam Tanzania.
Mshindi wa mpambano huu wa kukata na shoka atapata nafasi ya kupanda ulingoni kwenye mpambano wa utangulizi katika pambano litakalo wakutanisha wababe Floyd Mayweather na Manny Pacquiao.
Hili litakuwa ni pambano la 17 kwa Mohamed Matumla, tangu aanze ngumi za kulipwa akiwa ameshinda mara 11, amepoteza mara 4 na kutoka sare mara 2.
Pambano hili litatanguliwa na mapambano kadhaa ya awali kati ya Ashraf Suleiman wa Tanzania ataonyeshana umwamba na Joseph Rabotte wa Marekani katika pambano la uzito wa juu.
Kalama Nyarawila na Thomas Mashali, wote wa Tanzania watapambana katika uzito wa kati kuwania taji la WBF.
Huku Japhet Kaseba wakipepetana na Maada Maugo katika uzito wa Light kuwania ubingwa wa taifa.

MTOTO WA MIAKA 2,AWEKA REKODI INDIA.


Mtoto wa miaka 2 aweka rekodi India 
Amini usiamini mtoto mwenye umri wa miaka miwili ameweka rekodi ya taifa ya ulengaji shabaha kwa mishale nchini India.
Kulingana na vitabu vya kumbukumbu ya rekodi za taifa, Dolly Shivani Cherukuri kutoka Vijaywada katika jimbo la Andhra Pradesh
aliweka rekodi ya kuwa mshiriki mwenye umri mdogo zaidi kusajili alama 200 katika mashindano yaliyoandaliwa jumanne iliyopita.
Kulingana na jarida la Press Trust la India ,mtoto huyo alifuma mishale 36 kutoka umbali wa mita 5 na kisha umbali wa mita 7 na kujizolea alama 388.
Tukio hilo lilishuhudiwa na wachezaji wakongwe na maafisa kutoka idara ya kumbukumbu za michezo.
''kwa hakika tunajivunia matokeo haya ''alisema afisa wa shirikisho la mishale la India bwana Gunjan Abrol.
Dolly ambaye alizaliwa baada ya kupandikizwa kwa mbegu ya babake kufuatia kifo cha kakake katika ajali ya barabarani.

Mtoto wa miaka 2 aweka rekodi India
Kakake alikuwa mrushaji mishale wa kimataifa Cherukuri Lenin.
Babake Cherukuri Satyanarayana ,anasema kuwa Dolly alifunzwa kufuma mishale, tangu alipozaliwa.
Babake ni mmiliki wa klabu kimoja kinachofunza kurusha mishale.
Aidha aliiambia shrika la habari la AFP kuwa kitambo alikuwa amemptengezea uta na mishale nyepesi ilikukuza talanta ya mtoto huyo.
Sasa babake anasema kuwa anapanga kumshirikisha mwanawe katika mashindano kwa nia ya kumsajili katika vitabu vya rekodi za dunia za Guinness.
CHANZO BBC.

AWEKWA MOYO WA MTU ALIYE KUFA UINGEREZA.

Cambridgeshire
Madaktari wa upasuaji huko Cambridgeshire wamefanya upandikizaji wa kwanza wa moyo barani Ulaya kwa kutumia moyo mwengine uliosimama kufanya kazi.
Myoyo hiyo hupatikana kutoka kwa watu waliokufa lakini ambao myoyo yao bado inafanya kazi.
Katika upasuaji huo,moyo huo ulitoka kwa mtu ambaye mapafu yake na moyo wake ulikuwa haufanyi kazi.
Hospitali ya Papworth inasema kuwa mbinu hiyo huenda ikaongeza idadi ya myoyo inayopatikana kwa asilimia 25.
Mgonjwa aliyewekwa moyo mpya kwa jina Huseyin Ulucan, mwenye umri wa miaka 60, kutoka London,alikabiliwa na shinikizo la moyo mwaka 2008.
Alisema:kabla ya upasuaji,sikuweza kutembea na nilichoka sana,kwa hakika siku na maisha mazuri.

Upandikizaji wa moyo
Lakini anasema kuwa amefurahishwa na kuimarika kwa afya yake tangu upandikizaji huo.
Kwa sasa najisikia mwenye nguvu kila siku,na nimetembea hadi haospitalini asubuhi hii bila tatizo.
Kumekuwa na visa 171 vya upandikizaji wa myoyo katika kipindi cha miaka 12 iliopita nchini Uingereza.
Lakini mahitaji yanashinda myoyo iliopo ,hivyobasi wagonjwa wengine hungoja kwa miaka mitatu kupata kiungo kinachowafaa.
Wengi ya wagonjwa hao hufariki kabla ya kiungo kupatikana.
CHANZO BBC.

GWAJIMA AJISALIMISHA POLISI.

Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la Uzima na Ufufuo, Josephat Gwajima amejisalimisha kituo cha polisi kati kuhojiwa juu ya kutoa lugha chafu dhidi ya Askofu Mkuu wa Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Muadhama Polycarp Kardinali Pengo.
Akiongea kabla ya kuhojiwa na polisi Mchungaji Gwajima amejitetea kuwa alichofanya ni kutumia fursa ya kumuonya kiongozi mwenzake wa kiroho kutokana na kuwageuka wenzake katika makubaliano waliofikia katika tamko la kuipigia kura ya hapana Katiba inayopendekezwa.
Mchungaji Gwajima anadaiwa kumkadhifu na kumtukana hadharani Kardinali Pengo. Inadaiwa matusi hayo yameonekana kupitia mitandao mbalimbali ya kijamii ya WhatsApp na mingineyo, ambapo kuna sauti iliyorekodiwa na picha za video zikimuonyesha Mchungaji Gwajima akimkashifu na kumtukana kwa maneno makali Kardinali Pengo katika hali ambayo pia imewaudhi watu wengine.
CHANZO BBC.

FUNZA ZAIDI YA MIA MOJA WABAINIKA PUANI.

Funza hao walioondolewa puani kama wanavyoonekana.
Mwanamume mmoja amekutwa na kuondolewa funza wapatao mia moja walio hai tena wanao kula kula puani mwake na kuruhusiwa aende nyumbani .Mwanamume huyo anatajwa kuwa na umri wa miaka sitini na mitano ,na watabibu wanasema funza hao walikuwa wamejichimbia ndani zaidi ya pua yake.
Mwanamume huyo ni mwenye asili ya Sao Paulo, nchini Brazil,alikuwa akisumbuliwa mno na njia ya mfumo wa hewa hasa puani ,na pua yake ilikuwa imeathiriwa na mabuu ya inzi.
Pamoja na mambo mengine, mara kwa mara mwanaume huyo alikuwa akilalamika kuwa kuna minyoo pia huwa inadondoka kutoka puani mwake.
Tundu za pua ni mahali ambapo vijidudu virukavyo huweza kutaga mayai yao hapo na baadaye hugeuka kuwa funza.
Na wataalamu wa pua na koo wanasema kwamba chakula kikuu cha funza wakaao puani ni nyama za pua na endapo mgonjwa ataachwa bila kupatiwa matibabu ,funza hao wanauwezo wa kutafuna na kuharibu kabisa mfupa wa mwanzi wa pua,kuharibu vimishipa vya uso,pua na macho.
Na hali hiyo ikitokea,jua kutakuwa na maambukizi kwenye ubongo na macho na kwa kawaida husababisha ugonjwa wa uti wa mgongo na hata kifo.
Mwanaume huyo aliamua kwenda kwenye zahanati nchini Brazil kutoa malalamiko yake kwamba siku mbili nyuma aliona kitu kinachofanana na mnyoo ukichomoza na hatimaye kutoka katika pua yake upande wa kushoto.

Funza wakiwa puani
Mwanaume huyo anaishi na virusi vya ukimwi ana tatizo la ini,na kinga yake ya mwili ilikuwa inapungua kwa kasi kubwa na alikuwa hajaanza kutumia vidonge vya kurefusha maisha.
Miaka mitano iliyopita alifanyiwa upasuaji wa pua yake baada ya kugundulika kuwa alikuwa na uvimbe puani na hakuona dalili yoyote hapo kabla,ingawa kwa wiki nzima kabla ya kuhudhuria zahanati alikuwa akitokwa na damu puani,maumivu ya pua upande wa kushoto
Na harufu mbaya,alikuwa akishindwa kupumua sawa sawa na uvimbe ulianza kuonekana usoni na puani mwake.
Lakini baada ya kudumbukiza kijikamera kidogo puani mwake ,aligundulika
Madaktari wakaanza kuwatoa funza hao kwa muongozo wa kamera iliyokuwa ikiangaza puani na kuitibu pua yake.
Iliwachukua siku nne madaktari kuondoa uambukizo katika pua ya mwanaume huyo na baada ya hapo madhila yake yakakoma na baada ya uangalizi wa mwisho kwa kutumia kamera ile ile imethibitika kwamba tatizo lake lime kwisha.
CHANZO BBC.

EBOLA;RAIA WA S LEONE KUSALIA MAJUMBANI.

Raia wa Sierra Leone waanza kusalia majumbani kwa siku tatu kwa lengo la kukabiliana na ebola 
Mamlaka nchini Sierra Leone imeanza kutekeleza hatua ya kutotoka kwa siku tatu miongoni mwa raia wake itakayosaidia kukabiliana na kuenea kwa mlipuko wa ugonjwa wa ebola.
Takriban watu millioni sita wametakiwa kusalia majumbani mwao kwa kipindi cha siku tatu huku watu wa kujitolea wakitembelea nyumba hadi nyumba kuwasaka watu walio na ishara za ugonjwa huo huku wakiwashauri wengine jinsi ya kuepuka maambukizi.
Visa kadhaa bado vinaendelea kuripotiwa kazkazini na Magharibi mwa Sierra Leone kila wiki.
Mataifa matatu ya Afrika Magharibi yalioathiriwa vibaya na Ebola Sierra Leone,Liberia,Guinea-yameweka lengo la kutokuwa na hata kisa kimoja cha ebola ifikiapo katikati ya mwezi ujao.
CHANZO BBC.

NIERIA; JESHI LAICHUKUA NGOME YA B HARAM.

Jeshi la Nigeria lauteka mji wa Gwoza
Jeshi la Nigeria linasema kuwa limeuchukua mji wa kazkazini mashariki wa Gwoza unaoaminika kuwa ngome kuu ya Boko Haram.
Ni katika eneo hilo ambapo wapiganaji wa Boko Haram walitangaza uongozi wa kiislamu na ni miongoni mwa miji mikuu iliotekwa na kundi hilo katika kipindi cha hivi karibuni.
Tangazo hilo linajri siku moja tu kabla ya uchaguzi mkuu nchini Nigeria unaotarajiwa kuwa na ushindani mkubwa.
Uchaguzi huo uliahirishwa kwa mda wa wiki sita ili kutoa fursa kwa jeshi la muungano wa mataifa kupata mda zaidi wa kukabiliana na Boko Haram.
Rais wa Chad,taifa ambalo ni miongoni mwa yale yaliyo na vikosi vyake amesema kuwa vikosi vya Nigeria havijajizatiti.
CHANZO BBC.

RUBANI ALIKUWA NA MATATIZO YA AKILI.


Ajali ya ndege
Viongozi wa mashtaka nchini Ujerumani wanasema kuwa wamepata ushahidi unaosema kwamba rubani wa ndege ya Ujerumani ilioanguka katika milima ya ALPS na kuwaua abiria 150 alikuwa amemficha mwajiri wake kuhusu ugonjwa anaougua.
Maafisa hao pia wamesema kuwa walipata kijikaratasi cha ugonjwa kilichokuwa kimekatwa ambacho kilimtaka rubani huyo kupumzika siku ya kuanguka kwa ndege hiyo.

Maafisa wa Polisi wa ujerumani
Hatahivyo hawakupata ujumbe wowote wa rubani huyo kutaka kujitoa uhai wake.
Vyombo vya habari nchini Ujerumani vimeripoti kwamba faili ya rubani Andreas Lubitz mwenye umri wa miaka 27 katika shirika la anga za juu imeonyesha kuwa Andreas alikuwa na matatizo ya akili na alitakiwa kufanyiwa ukaguzi wa mara kwa mara.

Andreas Lubitz 
 Ripoti nyengine ambazo hazijathibitishwa zinasema kuwa alilazimika kuchukua likizo ya miezi sita kutoka kwa mafunzo ya urubani kutokana na shinikizo la akili.

Jumatano, 25 Machi 2015

MABIBI HARUSI WA ZAMANI ZIMBAMBWE WAONGOEA.

 
Raisi wa Zimbabwe Robert Mugabe
Mabibi harusi wa zamani wawili wameamua kuipeleka serikali ya Zimbabwe mahakamani katika harakati za kuvunja sheria kandamizi nchini humo na kutaka sheria inayoruhusu mabinti kuolewa wakingali wadogo iwe ni kinyume na katiba na si halali kwa kifupi iharamishwe.
Mabibi harusi hao Loveness Mudzuru na Ruvimbo Tsopodzi wamesema ndoa za utotoni ,ambazo ni ruksa nchini Zimbabwe,wansema ni sawa na ukatili wa kijinsia kwa watoto ambao huwanasa mabinti na kuishia katika janga la umasikini na madhila yasiyosemeka.
Nimekabiliana na changamoto zisizosemeka ,mume wangu alikuwa akinipiga sana.nilikuwa natamani kuendelea na masomo lakini yeye alikataa.nilikuwa na hali mbaya sana huu ni ushuhuda wa Tsopodzi, mama wa mtoto mmoja,mama huyu aliolewa akiwa na umri wa miaka kumi na mitano tu .
Na anaendelea kusema kwamba anataka kuchukua hatua hiyo ili kuleta tofauti,ameeleza hayo akiwa katika mji mkuu wa nchi hiyo Harare mapema wiki hii.Na hii yote ni katika harakati za kuzuia mabinti wadogo wanaoolewa katika umri mdogo.
Takwimu zilizochapishwa mwaka wa jana zinaonesha kwamba moja ya tatu ya wasicha walio na umri wa chini ya miaka kumi na nane huolewa , wakati wengine wapatao asilimia tano huolewa kabla ya kutimiza umri wa miaka kumi na mitano.
Katika tamko lao kwa mahakama ya katiba, Tsopodzi na Mudzuru, ambao kwa sasa wana miaka 19 na mwingine ana miaka 20, wanasema kwamba sheria ya ndoa nchini Zimbabwe ni ya kibaguzi kwani inamtaka mtoto wa kike aolewe akiwa na umri wa miaka kumi na sita wakati mtoto wa kiume anatakiwa kuoa akishatimiza umri wa miaka kumi na nane, na ndoa za kimila hazijaainisha umri halisi wa kijana ama binti kuoa ama kuolewa.
Sheria ya ndoa ya mwaka 2013 inasema kwamba kila mtoto mwenye umri wa miaka kumi na mitatu,anayo haki ya kupata malezi ya wazazi,elimu na ulinzi kutoka kwao katika masula ya unyonyaji kingono na kiuchumi.
Sheria hii pia haijaweka wazi umri wa kuoa ama kuolewa lakini inasisitiza kwamba hakuna mtu yeyote atakayelazimishwa kuoa ama kuolewa kinyume na matakwa yao na kuonesha wazi kuwa raia wa Zimbabwe mwenye umri wa miaka kumi na nane anaweza kuwa na familia yake.
Umasikini ndio chanzo cha ndoa za utotoni nchini Zimbabwe na kuwasababisha kuolewa kabla ya umri wao wasichana walio wengi ,na hivyo kuwasababisha wazazi kupunguza mzigo wa familia katika masuala ya matunzo na kubakisha mama tu na baba.ulipwaji mahari nayo ni motisha inayowafanya wazazi kutowatendea haki watoto wao.
Baadhi ya familia nchini Zimbabwe zinatukuza ndoa za utotoni kwa mtazamo wa kuwalinda watoto wao wa kike na ngono kabla ya ndoa.
Mudzuru anatoa ushuhuda wake kwamba ndoa za utotoni ni chagamoto kubwa ,kwani mabinti hao walio katika umri mdogo watazaa watoto wakiwa katika familia masikini na hapo ndipo mzunguuko wa ndoa za utotoni unapoanza upya.
Mudzuru, aliolewa akiwa na umri wa miaka kumi na sita kwa sasa ana watoto wawili tena akiwa hajatimiza miaka kumi na nane ,anasema maisha yake yalikuwa sawa na jehanamu ya moto na aliishi maisha yake katika dhiki isiyosemeka.
Nasema maisha yake yalikuwa magumu sana, kulea watoto ilhali wewe mwenyewe ukiwa ni mtoto ni vigumu,na asema katika umri wake alipaswa kuwa anahudhuria masomo shuleni.
Naye mwanasheria wa mabinti hao ambao ni akina mama sasa hivi,alikuwa ni waziri wa zamani wa fedha nchini humo Tendai Biti, aliwasilisha changamoto hizo za kisheria mwezi January mwaka huu.
Beatrice Savadye,yeye ni mwanaharakati wa kupinga ndoa za utotoni nchini humo anayeongoza asasi isiyokuwa ya kiserikali,ijulikanayo kaka ROOTS ,asasi ambayo inawaunga mkono akina mama hao wawili anasema kesi hiyo imekuwa na mvuto wa kipekee nchini humo nan je ya nchi hiyo kwa ujumla wake.
Na anamashaka kama mahakama itatoa maamuzi yake lini ,lakini inalazimika kutoa maamuzi yake ndani ya miezi sita.

Wazimbabwe
Ulimwenguni kwa ujumla wake wasichana milioni kumi na tano wanaolewa kila mwaka.katika jangwa la sahara peke yake asilimia arobaini ya wanawake huolewa wakiwa katika umri mdogo.
chanzo bbc.

AFANDE ATANGAZA NIA YA KUGOMBEA UBUNGE KUPITIA ACT


Mwanamuziki wa kizazi kipya, Suleimani Msindi ‘Afande sele’, ametangaza nia ya kuwania ubunge wa Morogoro mjini kupitia Chama cha Alliance for Change and Transparency (ACT-Tanzania). Msanii huyo ametangaza azma yake baada ya kujiunga na chama hicho akitokea Chama cha Chadema.

YANGA YATUMIA SALAMU PLATINUM FC.

Furaha ya ushindi ya Yanga
Yanga ya Tanzania imeitumia salamu timu ya Platinum FC ya Zimbabwe kufuatia ushindi mfululizo katika ligi kuu ya Tanzania Bara.
Yanga imeifunga JKT Ruvu 3-1 katika ligi kuu Tanzania Bara, huku Danny Mrwanda, aliyewahi kucheza soka huko Vietnam akifunga goli moja na Simon Msuva akitupia mawili katika uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam. Hivi karibuni, Yanga pia iliwafunga Mgambo Shooting 2-0 ikiwa ni mfululizo wa ushindi katika mechi zake
Mechi hizo ni sehemu ya maandalizi kwa safari ya Yanga kuelekea Zimbabwe kurudiana na Platinum FC katika mechi ya kombe la Shirikisho barani Afrika mapema mwezi ujao.
Yanga ilishinda 5-1 katika mechi ya awali ikiwa uwanja wa nyumbani na inahitaji ushindi wa aina yoyote, droo au hata ikifungwa magoli yasiyozidi 4 ili isonge mbele kunusa hatua ya 16 bora.
Yanga kwa sasa inaongoza ligi kuu Tanzania Bara ikiwa a pointi 40 katika michezo 19 iliyocheza huku Azam ikifuatia ikiwa na pointi 36 katika michezo 18 iliyocheza.
CHANZO BBC.

MLINZI WA LIVERPOOL APIGWA MARUFUKU.

Mlinzi wa Liverpool Martin Skrtel 
Mlinzi wa kilabu ya Liverpool Martin Skrtel atahudumia marufuku ya mechi tatu baada ya kamati ya nidhamu ya shirikisho la soka nchini Uingereza FA kukataa ombi lake la kukata rufaa dhidi ya hatua ya kinidhamu dhidi yake.
Raia huyo wa Slovak alimkanyaga kipa wa Manchester United David de Gea katika dakika za lala salama za ushindi wa 2-1 wa Manchester United dhidi ya Liverpool katika uwanja wa Anfield siku ya jumapili.
Tukio hilo halikuonekana na refa Martin Atkinson.
Skrtel mwenye umri wa miaka 30 alisema kuwa kisa hicho hakikuwa cha makusudi.
Hatahivyo kamati hiyo ya nidhamu ilikataa ombi hilo hatua ambayo itamfanya mchezaji huyo kukosa mechi tatu za EPL huko Arsenal,Newcastle, pamoja na robo fainali ya kombe la FA dhidi ya Blackburn.
CHANZO BBC

NIERIA YAKIRI KUTEKWA NYARA KWA RAIA.

Serikali ya Nigeria yakiri kutekwanyara kwa baadhi ya raia na Boko Haram
Serikali ya Nigeria imekiri kwamba raia,wakiwemo watoto wametekwa nyara na wapiganaji wa Boko Haram katika majuma ya hivi karibuni.
Msemaji Mike Omeri amesema kuwa ni vigumu kukisia idadi ya watu ambao wametekwa wakati wapiganaji wa Boko Haram wakitoroka wakati wa mashambulizi dhidi yao yanayotekelezwa na vikosi vya kijeshi kutoka Nigeria,Chad na Niger.
Lakini msemaji wa Nigeria alipinga madai kwamba zaidi ya watoto 500 walikuwa hawajulikani waliko kutoka mji uliochukuliwa na jeshi Damasuk karibu na mpaka wa Niger.
Nigeria imetangaza kwamba inafunga mpaka wake kuanzia siku ya jumatano usiku hadi jumapili huku uchaguzi wa urais ukifanywa.
CHANZO BBC.

MAREKANI KUSHAMBULIA IS MJINI TIKRIT.

Rais wa Iraq Fouad Massoum 
Rais wa Iraq Fouad Massoum ametoa ishara kwamba jeshi la muungano linaloongozwa na Marekani huenda likatekeleza mashambulizi dhidi ya wapiganaji wa Islamic State mjini Tikrit.
Katika kipindi cha siku chache zilizopita, muungano huo ulianza kufanya uchunguzi katika mji huo wa Iraq.
Bwana Massoum ameliambia shirika la habari la Reuters kwamba baada ya kukusanya ripoti za uchunguzi wa ndege,muungano huo utaanza oparesheni za kijeshi.
Hadi kufikia sasa ,Marekani imejiondoa katika jaribio la vikosi vya Kishia vya Iran kuuteka mji wa Tikrit.
Hatahivyo jaribio hilo limefeli huku mamia ya wapiganaji wa ISIS wakisalia katikati ya mji.
Rais wa Iraq hajasema iwapo serikali ilitaka mashambulizi ya angani ya Marekani katika mji wa Tikrit.
CHANZO BBC.

ROBO YA WASUDANI KUSINI WAMEATHIRIKA NA NJAA.


Robo ya wasudan Kusini wameathirika na njaa 
Zaidi ya watu milioni mbili unusu wanahitaji chakula cha msaada cha dharura, baada ya kufurushwa makwao kutokana na mapigano kati ya jeshi la serikali na vikosi vya waasi.
Mazungumzo ya kuleta amani yaliyokuwa yakiendelea katika taifa jirani la Ethiopia, yamesambaratika.
Haya yanajiri siku moja tuu baada ya bunge kumuongeza rais Salva Kiir miaka mitatu zaidi afisini na kuhairisha uchaguzi uliotarajiwa mwaka huu.
Mwandishi wa BBC Emmanuel Igunza anaelezea zaidi.
Hapa ni katika mji wa Ganyiel kwenye jimbo lenye utajiri mkubwa wa mafuta la Unity, maelfu ya watu waliofurushwa makwao wamefika katika kituo cha Shirika la WFP
ambapo wanapata mtama, mafuta na chumvi.
Kwa wengi hapa msaada huo ndio chakula cha pekee wakatachopata.
Shirika la WFP linasema mtu mmoja kati ya wane nchini humo, hawajui watapata wapi chakula
Nchi hii iliepuka kiangazi mwaka uliopita, lakini bado hakuna chakula cha kutosha.

Asilimia kubwa ya raia wa Sudan Kusini wanahitaji chakula cha dharura
WFP inasema watu milioni mbili unusu wanahitaji msaada wa dharura na idadi hiyo huenda ikaongezeka mara mbili kufikia katikati ya mwaka huu, iwapo mapigano yataendelea.
Miongoni mwa wanaopanga foleni hapa kutafuta chakula ni Elizaberth Nyalat aliyetoroka mapigano katika mji wa Nyalat, Kusini Magharibi mwa Nchi hiyo.
"nilikuwa nasomea mjini Yei, wakati vita vilipoanza.
Nilitoroka Yei hadi hapa.
Lakini sio kwa gari wala boti, nilikimbia kwa miguu.
Ilikuwa ngumu sana kwangu kufik amahali hapa."
Lakini amani hiyo imekuwa ngumu kupatikana. Baada ya miezi kumi na mitano ya mapigano yaliyofanya maeneo mengi kaskazini mwa nchi hiyo kuwa numu kuyafikia.
Na sasa mashirika ya kutoa misaada yako mbioni kutoa usaidizi kabla ya msimu wa mvua kuanza. Ertharin Cousin ni mkurugenzi Mkuu wa WFP
"watu milioni tatu tunaojaribu kuwafikia,sio tu takwimu ni watu wa kweli.

Asilimia kubwa ya raia wa Sudan Kusini wanahitaji chakula cha dharura
Tatizo ni kuwa , vita hivi vinavyoendelea kwa muda mrefu, ndivyo watu hawa wanasahaulika na kutazamiwa tu kama gharama au takwimu tu.
Lakini haya ni maisha ya watu. Ni binadamu."
Awamu mpya ya mazungumzo ya amani yanatarajiwa kuanza tena mwezi ujao...lakini huenda ikaathirika na hatua ya bunge hapo jana kumuongezea Rais Kiir miaka mitatu zaidi mamlakani.
Uchaguzi wa mwezi Juni pia umeahirishwa.
Upinzani hata hivyo unasema hatua hiyo ya Kiir ni sawa na kukwamilia mamlaka.
Na huenda ikavuruga juhudi nzima ya kuleta amani nchini humo.
CHANZO BBC.

UKANDA WA KATI WAPANIA KUKUZA UCHUMI.


Injini ya treni ya mizigo ya kampuni ya Reli Tanzania, TRL 
Marais wa Afrika Mashariki na kati wamezindua rasmi mradi wa mabehewa mapya ya mizigo yatakayokuwa yakisafirisha mizigo kutoka bandari ya Dar es Salaam nchini Tanzania kwenda katika nchi za Rwanda, Uganda, Burundi na Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo ili kuimarisha ushirikiano wa kiuchumi katika eneo hilo.
Uzinduzi huo umefanyika Jumatano ambayo ni siku ya kwanza ya mkutano wa siku mbili unaotarajiwa kuhudhuriwa na marais wote wa nchi hizo, hata hivyo mpaka mkutano huo unaanza ni Rais Yoweri Museveni wa Uganda na Pierre Nkurunzinza wa Burundi pamoja na mwenyeji wao Rais Jakaya Kikwete ndio waliokuwa wamehudhuria, huku Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya, Paul Kagame wa Rwanda na Joseph Kabila wa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo wakituma wawakilishi wao.
Akizungumza katika mkutano wa viongozi wa nchi hizo na wawakilishi wa mashirika na taasisi za fedha na wawekezaji jijini Dar es Salaam, Rais wa Tanzania Jakaya Kikwete amesema nchi yake imedhamiria kuimarisha ushirikiano wa kiuchumi na nchi za eneo la ukanda wa kati kwa kuboresha miundombinu ya barabara na reli na kupunguza kwa kiasi kikubwa urasimu katika utoaji wa huduma za bandari na vikwazo vya barabarani.

Uzinduzi wa Treni ya Mizigo kwenda nchi za Rwanda, Uganda, Burundi na Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo kutoka Dar es Salaam, Tanzania.
Tatizo la uchelewashaji mizigo katka bandari ya Dar es Salaam ni suala ambalo kwa muda mrefu limekuwa likilalamikiwa na watumiaji wa bandari hiyo. Hata hivyo, sasa limeanza kupatiwa ufumbuzi ambapo Katibu Mkuu wa wizara ya Uchukuzi nchini Tanzania Dakta Shaban Mwijaka amesema muda wa utoaji wa mizigo katika bandari ya Dar es Salaam umepungua kwa kiasi kikubwa kutoka siku 20 hadi siku tatu, sababu kubwa akisema ni matumizi ya mfumo wa kielektroniki badala ya kutumia makaratasi.
Nchi za Afrika mashariki na kati zimepiga hatua katika uimarishaji wa miundombinu ya barabara, hata hivyo rais Yoweri Museveni wa Uganda ameonya kwamba juhudi hizi hazitakuwa na tija iwapo juhudi zaidi hazitafanyika katika kuboresha miundombinu ya reli. Pia Rais Museveni amesema uvivu, rushwa na kutowajibika ni mambo yanayokwamisha ustawi wa maisha ya watu wa kawaida katika eneo hilo na Afrika kwa jumla.
Marais hao pia wamekagua miundombinu ya bandari, na kuitaka mamlaka ya bandari ya Dar es Salaam kuongeza ufanisi zaidi ili kuvutia wawekezaji katika sekta ya usafirishaji na miundombinu.
chanzo bbc.