Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Jumanne, 17 Machi 2015

MAKINDA: BUNGE LINAMTAMBUA ZITTO KABWE KAMA MBUNGE

 
MH.ANNE MAKINDA.
Spika wa Bunge Mh Anne Makinda amesema kuwa kwa niaba ya Bunge bado anamtambua mbunge wa 
Kigoma Kaskazini Zitto Kabwe kuwa ni mbunge halali wa bunge hilo.
Akizungumza nje ya ukumbi wa bunge mara baada ya kikao cha Bunge kumalizika jana majira ya saa 5 Asubuhi, Makinda amesema kuwa anasubiri barua rasmi kutoka Tume ya Taifa ya Uchaguzi, ambayo ndiyo itakayompa mwongozo kuhusu ubunge wa Zitto Kabwe.
Amesema kwa mujibu wa taratibu, kama chama kikimvua uanachama mbunge, kinapaswa kuiandikia Tume ya Taifa ya Uchaguzi, ambayo nayo inatoa mwongozo kwa bunge, jambo ambalo halijafanyika hadi sasa.
Kwa upande wake Mwanasheria Mkuu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo Mh. Tundu Lissu alipoulizwa kuhusu suala hilo amesema kuwa anayetakiwa kuandika barua hiyo ni Katibu Mkuu wa Chama, na si yeye na kwamba hajapata taarifa kama barua hiyo imeandikwa au la..!
Licha ya kuendelea kutambuliwa na uongozi wa Bunge, Zitto Kabwe leo hakuhudhuria kikao hicho cha Kwanza cha mkutano wa 19 wa bunge la 10.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni