Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Jumanne, 24 Machi 2015

TUNISIA;MAKAZI YAFUNGULIWA LEO.

 
Hapo jana waziri mkuu wa taifa hilo aliwalaumu maafisa wakuu wa idara za usalama kwa kuzembea kazini 
Makavazi ya Bardo nchini Tunisia, yanafunguliwa tena leo Jumanne, juma moja pekee baada ya magaidi kushambulia watalii wa kigeni na kuwauwa 20 kati yao.
Kutakuwa na mkutano wa hadhara kabla ya kufunguliwa tena kwa makavazi hayo ya kitaifa.
Wasanii watawatumbuiza wageni nje ya ukumbi huo unaopendwa na watalii wengi kutoka magharibi kabla ya maafisa kutoa taarifa inayolenga kuthibitisha kuwa magaidi hawataamua maisha ya wenyeji yasalie kuwa ya hofu.
Tangu tukio hilo kumekuwa na hofu kuwa magaidi hao huenda wameangamiza sekta nzima ya utalii ambayo ni kitega uchumi kikubwa cha Tunisia.
Hapo jana waziri mkuu wa taifa hilo aliwalaumu maafisa wakuu wa idara za usalama kwa kuzembea kazini .
Sita kati yao walitupwa nje.

Maafisa wa usalama wakishika doria nje ya makavazi hayo ya kitaifa
Waziri huyo mkuu , Habib Essid alisema mikakati imewekwa ilikuimarisha uwezo wa maafisa wa usalama kushirikiana na vitengo vya kijasusi kuzuia mashambulizi zaidi siku za usoni.
Jumba hilo linashehena kubwa zaidi ya sanamu za enzi za warumi.
Wavamizi wawili kati ya watatu waliotekeleza shambulizi hilo walipigwa risasi na kuuawa huku yule aliyesalia akisakwa na maafisa wa kitengo maalum cha kupambana na ugaidi.
Tukio hilo ndilo kubwa zaidi kuwahi kutokea baada ya mapinduzi ya kiongozi wa muda mrefu wa Tunisia Zine al-Abidine Ben Ali mwaka wa 2011.
CHANZO  BBC.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni