Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Jumatano, 25 Machi 2015

NIERIA YAKIRI KUTEKWA NYARA KWA RAIA.

Serikali ya Nigeria yakiri kutekwanyara kwa baadhi ya raia na Boko Haram
Serikali ya Nigeria imekiri kwamba raia,wakiwemo watoto wametekwa nyara na wapiganaji wa Boko Haram katika majuma ya hivi karibuni.
Msemaji Mike Omeri amesema kuwa ni vigumu kukisia idadi ya watu ambao wametekwa wakati wapiganaji wa Boko Haram wakitoroka wakati wa mashambulizi dhidi yao yanayotekelezwa na vikosi vya kijeshi kutoka Nigeria,Chad na Niger.
Lakini msemaji wa Nigeria alipinga madai kwamba zaidi ya watoto 500 walikuwa hawajulikani waliko kutoka mji uliochukuliwa na jeshi Damasuk karibu na mpaka wa Niger.
Nigeria imetangaza kwamba inafunga mpaka wake kuanzia siku ya jumatano usiku hadi jumapili huku uchaguzi wa urais ukifanywa.
CHANZO BBC.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni