Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Alhamisi, 19 Machi 2015

RAIA WA S LEONE KUTOKA NJE SIKU 3.

Ebola nchini Sierra Leone 
Katika harakati za kuangamiza kabisa janga la ugonjwa wa Ebola nchini Sierra Leone, taifa hilo linasema kuwa juma lijalo litawazuilia karibu watu milioni mbili unusu majumbani mwao kwa siku tatu.
Msemaji wa serikali ameiambia BBC kuwa shughuli hizo zitaanzia mji mkuu Freetown na kazkazini mwa nchi hiyo, kati ya Machi 27 na 29.
Wafanyikazi wa kimatibabu watazuru kila nyumba ili kubaini dalili za ugonjwa huo, huku wakiwakumbusha wananchi hatari ya kushika maiti na kuwapeleka wagonjwa wa ebola kwa madktari wa tiba ya kiasili.
Visa vya Ebola vinaripotiwa kila juma nchini Sierra Leone na Guinea.
Kufikia sasa hakuna kisa chochote cha ugonjwa huo ambacho kimeripotiwa nchini Liberia, katika kipindi cha majuma matatu yaliyopita.
chanzo  bbc.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni