Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Jumanne, 31 Machi 2015

OBAMA KUZURU KENYA JULAI.


Obama kuzuru Kenya Julai 
Ikulu ya Marekani imetangaza kuwa, Rais Barrack Obama atazuru Kenya mwezi Julai mwaka huu, taifa alikozaliwa babake.
Inasemekana kuwa Bwana Obama, atahudhuria mkutano mkubwa wa kimataifa kuhusu ujasirimali, utakaofanyika katika mji mkuu wa nchi hiyo-Nairobi.
Tangu awe Rais wa Marekani, Barack Obama hajawahi kuzuru taifa hilo la Afrika Mashariki kama Rais.

Obama, atahudhuria mkutano mkubwa wa kimataifa kuhusu ujasirimali
Alizuru mataifa kadhaa za Afrika ikiwemo ziara ya taifa jirani Tanzania mnamo mwaka 2013 bila kuzuru Kenya.
Alizuru Kenya akiwa seneta mnamo mwaka 2006.
Bababke Obama alisomea Marekani na hatimaye kurejea Kenya baada ya Obama kuzaliwa.
chanzo bbc.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni