Furaha ya ushindi
Katika mapigano makubwa na makali
yanaondelea dhidi ya wanamgombo wa Islamic State, majeshi ya Iraq na
yale Shia yamezidi kupata ushindi na kuurudisha tena mji wa Tikrit.
Majeshi
ya nchi hiyo yamesema imewachukua usiku mzima kupambana katika eneo la
kaskazini, mashariki na magharibi kando ya mji, kuingian katikati mwa
mji.Kwa mujibu wa ripoti moja, kwa sasa wapiganaji mia moja na hamsini wa kundi la Islamic State wameendelea kuwepo katika mji huo wa Tikrit, ambao ni makao makuu ya jimbo la Salahuddin.
Mkuu wa operesheni za kijeshi katika jimbo hilo Luteni Jenerali Abdul-Wahab al Saadi amesema operesheni hiyo itaendelea mpaka wapiganaji hao wa Islamic State watakapoondolewa.
''...Mapambano kuusafisha mji wa Tikrit yanaendelea, tumeanzisha operesheni kadhaa za kijeshi- kiasi cha operesheni tano au sita hivi.
Wakati huu tunapozungumza operesheni za kijeshi zinaendelea na zitaendelea mpaka tutakapolikomboa jimbo zima la Salahuddin. Mungu akipenda...''
Akizungumza katika Chuo Kikuu cha Baghdad, Waziri mkuu wa Iraq, Haider al Abadi, ameelezea kufurahishwa kwake kutokana na majeshi ya nchi hiyo kuendelea kupata ushindi dhidi ya wapiganaji hao wa Islamic State, mjini Tikrit.
Ushindi mkubwa tulioupata ni kuunganisha nchi, umoja kwa ajili ya kuushinda ugaidi katika ardhi ya Iraq, kuwashinda wote wanaotaka kuwadhuru watoto wetu, nchi yetu na watu wetu. Huu ni ushindi halisi tulioupata leo...''.
CHANZO BBC
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni