Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Jumatano, 25 Machi 2015

YANGA YATUMIA SALAMU PLATINUM FC.

Furaha ya ushindi ya Yanga
Yanga ya Tanzania imeitumia salamu timu ya Platinum FC ya Zimbabwe kufuatia ushindi mfululizo katika ligi kuu ya Tanzania Bara.
Yanga imeifunga JKT Ruvu 3-1 katika ligi kuu Tanzania Bara, huku Danny Mrwanda, aliyewahi kucheza soka huko Vietnam akifunga goli moja na Simon Msuva akitupia mawili katika uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam. Hivi karibuni, Yanga pia iliwafunga Mgambo Shooting 2-0 ikiwa ni mfululizo wa ushindi katika mechi zake
Mechi hizo ni sehemu ya maandalizi kwa safari ya Yanga kuelekea Zimbabwe kurudiana na Platinum FC katika mechi ya kombe la Shirikisho barani Afrika mapema mwezi ujao.
Yanga ilishinda 5-1 katika mechi ya awali ikiwa uwanja wa nyumbani na inahitaji ushindi wa aina yoyote, droo au hata ikifungwa magoli yasiyozidi 4 ili isonge mbele kunusa hatua ya 16 bora.
Yanga kwa sasa inaongoza ligi kuu Tanzania Bara ikiwa a pointi 40 katika michezo 19 iliyocheza huku Azam ikifuatia ikiwa na pointi 36 katika michezo 18 iliyocheza.
CHANZO BBC.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni