Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Jumanne, 17 Machi 2015

KUNYONYESHA MUDA MREFU NI FAIDA.

 
Mtoto anayonya maziwa ya mama 
Utafiti uliofanyika nchini Brazil umebaini kuwa watoto wanaonyonya kwa muda mrefu wanakuwa na akili zaidi,wasomi,na wenye uwezo kifedha wanapokuwa watu wazima.
Ripoti ya utafiti huo iliyochapishwa katika jarida la afya la Lancet Global Health unafuatilia makuzi ya mtoto hadi kuikia utu uzima wake.
Wataalam hao wanasema kwa mtoto anayenyonya kwa takriban mwaka mmoja anakuwa na kiwango cha akili cha juu zaidi ya yule ambaye hajanyonya kwa muda huo kwa kiwango cha IQ cha mara nne zaidi.
Katika maziwa ya mama kwa mjibu wa wataalam hao kuna madini mhimu ambayo husaidia ukuaji wa ubongo na kuongeza kiwango cha ufahamu.
Hata hivyo utafiti wa safari hii kwa mjibu wa wataalam hao nikwamba una uhakika zaidi kwani walitumia kubwa ya watoto tofauti na idadi iliyotumika awali miaka 1980.
CHANZO BBC.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni