Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Alhamisi, 12 Machi 2015

MKENYA ACHAULIWA MAKAMUWA RAIS WA ICC

 
Justice Joyce Aluoch kutoka Kenya kushoto 
Majaji wa mahakama ya kimataifa kuhusu uhalifu wa kivita ICC wamemchagua jaji wa Kenya Joyce Aluoch kama makamu wa rais wa mahakama hiyo kwa kipindi cha miaka mitatu.
Kufuatia uchaguzi huo uliofanywa siku ya jumatano,Jaji wa Argentina Silvia Fernandez de Gurmendi alichaguliwa rais wa mahakama hiyo huku jaji Kuniko Ozaki kutoka Japan akichaguliwa kama makamu wa rais wa pili.
Urais wa Mahakama hiyo unawashirikisha rais na makamu wake wawili na unatoa mwongozo wa mahakama hiyo kwa jumla.
Rais wa ICC huwa mratibu wa mahakama hiyo na idara nyengine na hutoa mawaidha kwa kiongozi wa mashtaka kuhusu maswala yanayoleta wasiwasi kwa heshima ya mahakama hiyo.
Kulingana na mkataba wa Roma ,uongozi wa mahakama hiyo ya ICC ,unasimamiwa na rais huyo bila kumshirikisha kiongozi wa mashtaka.
CHANZO BBC.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni