Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Jumamosi, 21 Machi 2015

J OODLUCK; TUTALIMALIZA BOKO HARAM.

 
Goodluck Jonathan
Rais wa Nigeria, Goodluck Jonathan amesema ana matumaini kwamba katika muda wa mwezi mmoja kundi la wapiganaji wa kiislamu Boko Haram halitodhibiti sehemu yoyote.
Wanamgambo hao waliokiri ushirikiano na kundi la Islamic State liliziteka sehemu kubwa ya eneo la kaskazini mashriki mwa Nigeria.
Lakini operesheni ya kieneo imesadia serikali kudhibiti miji na vijiji kadhaa.
Rais Jonathan anayewania kuchaguliwa tena katika siku nane zijazo ametetea jitihada zake za kukabiliana na ukosefu wa usalama na amesema anaamini atashinda katika uchaguzi huo.
Kiongozi huyo amesema Boko Haram linazidi kuwa dhaifu na litasamabaratishwa.
Ameeleza kwamba silaha mpya ilizopata nchi hihyo pamoja na ushirikiano na nchi jirani zimesaidia kuwasukuma wanamgambo hao nje ya miji na vijiji.
Alipoulizwa ni wapi walikokimbilia, alieleza kwamba wakati wengi wamemiminika katika mipaka ya nchi hiyo, anadhani wengine wamekimbilia katika msitu wa Sambisa ulio ngome yao kaskazini mashariki mwa Nigeria.
chanzo bbc.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni