Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Jumatano, 25 Machi 2015

MLINZI WA LIVERPOOL APIGWA MARUFUKU.

Mlinzi wa Liverpool Martin Skrtel 
Mlinzi wa kilabu ya Liverpool Martin Skrtel atahudumia marufuku ya mechi tatu baada ya kamati ya nidhamu ya shirikisho la soka nchini Uingereza FA kukataa ombi lake la kukata rufaa dhidi ya hatua ya kinidhamu dhidi yake.
Raia huyo wa Slovak alimkanyaga kipa wa Manchester United David de Gea katika dakika za lala salama za ushindi wa 2-1 wa Manchester United dhidi ya Liverpool katika uwanja wa Anfield siku ya jumapili.
Tukio hilo halikuonekana na refa Martin Atkinson.
Skrtel mwenye umri wa miaka 30 alisema kuwa kisa hicho hakikuwa cha makusudi.
Hatahivyo kamati hiyo ya nidhamu ilikataa ombi hilo hatua ambayo itamfanya mchezaji huyo kukosa mechi tatu za EPL huko Arsenal,Newcastle, pamoja na robo fainali ya kombe la FA dhidi ya Blackburn.
CHANZO BBC

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni