Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Jumanne, 31 Machi 2015

HABARI ZA HIVI PUNDE;BUHARI ANUSIA USHINDI WA URAIS NIGERIA.

Jenerali Muhammadu Buhari anaongoza kwa zaidi ya kura milioni mbili zaidi ya mpinzani wake wa karibu ambaye ni rais Goodluck Jonathan
Huku yakisalia majimbo machache, Buhari anaongoza kwa karibu kura milioni tatu mbele ya Rais wa sasa Goodluck Jonathan.
Awali kulikua na matukio ya kurushiana maneno katika ukumbi mkuu wa hesabu ya kura pale mwakilishi wa chama tawala-PDP Elder Orubebe alipolalamikia tume ya uchaguzi kwa kupendelea.
Kumekua na kurushiana cheche za maneno makali katika ukumbi mkuu wa kuhesabu kura nchini Nigeria.
Mwakilishi wa chama tawala PDP-Elder Orubebe, alivuruga shughuli ya kutangazwa matokeo ya kura akidai tume ya uchaguzi ilikua ikipendelea upande mmoja.
 
Mawakala wa wagombeaji wakuu
Mwenyekiti wa tume ya kitaifa ya uchaguzi mkuu Nchini Nigeria, Attahiru Jega, alimuonya Elder Orubebe kuwa mwaangalifu kutokana na matamshi yake hayo aliyotoa.
Mwandishi wa BBC aliyeko ukumbi huo mjini Abuja anasema huenda vurugu hizo ni ishara kuwa, PDP inahisi kushindwa.
Huku majimbo mengi yakitoa matokeo yake mgombea wa upinzani, Muhammadu Buhari wa chama cha APC, anaendelea kuongoza kwa wingi wa kura, huku akifuatiwa na Rais Goodluck Jonathan.
Generali Buhari wa chama cha All Progressives Congress (APC) anaonekana kusajili matokeo mema mapema hata kabla ya kuhesabiwa kwa kura za mjini Lagos.
Matokeo ya uchaguzi mkuu nchini Nigeria yanatarajiwa kutangazwa saa chache zinazokuja wakati
majimbo yaliyosalia yakisubiriwa kutangaza matokeo yao.

Tume ya uchaguzi imesema itaendelea kutangaza matokeo ya uchaguzi Jumanne
Mwandishi wa BBC mjini Abuja amesema mchuano bado ni mkali.
CHANZO BBC.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni