Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Alhamisi, 12 Machi 2015

POLISI WAWILI WAJERUHIWA MJINI FERGUSON

 
 Polisi mjini Ferguson wameshutumiwa kutenda kazi kwa ubaguzi
Maafisa Polisi wawili wameshambuliwa kwa risasi mjini Ferguson, mji ambao umekuwa katika hali ya wasiwasi mwingi tangu kijana mweusi alipouawa na askari wa kizungu mwezi Agosti.
Afisa mmoja alipigwa usoni mwingine alijeruhiwa begani.Polisi wanasema wote wanapata matibabu hospitalini.
Shuhuda wa tukio hilo ameiambia BBC kuwa aliwaona maafisa wakiwa wametapakaa damu.
Shambulio la risasi lilitokea nje ya jengo la idara ya Polisi, ambako waandamanaji kadhaa walikusanyika baada ya Mkuu wa Polisi mjini humo Thomas Jackson alipotangaza kujiuzulu.
Idara ya Polisi ilikosolewa kuwa tukio la kuuawa kwa kijana huyo lilikua na viashiria vya ubaguzi wa Rangi.
Afisa mkuu wa utawala wa eneo la Furguson na Jaji wa manispaa ya mji huo walijiuzulu mwanzoni mwa juma hili.
chanzo bbc

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni