Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Alhamisi, 19 Machi 2015

MAPIGANO MAKALI YASHUHUDIWA YEMEN.

 
 Mapigano makali yashahudiwa katika uwanja wa ndege Yemen
Mapigano makali yanashuhudiwa nje na ndani ya uwanja wa ndege katika mji wa Aden nchini Yemen.
Taarifa zinasema maafisa wa polisi waaminifu kwa aliyekuwa rais wa nchi hiyo, Ali Abdullah Saleh, walishambulia sehemu moja ya uwanja wa ndege, lakini wakakabiliwa na makundi ya usalama yanayomuunga mkono rais wa sasa, Abed Rabbo Mansour Hadi.
Milipuko kadhaa imetokea katika uwanja huo na abiria waliagizwa kushuka kwenye ndege iliyokuwa inatarajiwa kuondoka kuelekea Cairo.
Washambuliaji watatu waliuwawa katika mapigano huku kumu kati yao wakitiwa mbaroni.
Aden ni ngome kuu ya rais Abdrabbuh Mansour Hadi, aliyekwepa nyumbani alikokuwa anazuiliwa katika mji mkuu Sanaa baada ya waasi wa madhehebu ya kishia - Houthi kulidhibiti kikamilifu eneo hilo mnamo mwezi Januari.
chanzo bbc.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni