Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Jumamosi, 21 Machi 2015

KISA KIPYA CHA EBOLA CHAPATIKANA LIBERIA.

Mgonjwa wa Ebola Yardolo akituhusiwa kwenda nyumbani 
Kisa kipya cha ugonjwa wa ebola kimegunduliwa nchini Liberia wiki chache kabla ya nchi hiyo kutangazwa kuwa isiyokuwa na ugonjwa huo.
Mkuu wa kundi linalohusika na kudhibiti ugonjwa wa ebola nchini humo ameiambia BBC kuwa mwanamume mmoja ambaye alipelekwa kwenye kituo cha matibau siku ya alhamisi alipatikana akiwa na ugonjwa wa ebola.
Wiki mbili zilizopita mgonjwa wa mwisho wa ugojwa wa ebola (Beatrice Yardolo) aliruhusiwa kuondoka hospitalini kwenye mji mkuu wa nchini hiyo Monrovia.
Liberia ilikuwa imesalia na siku 40 kabla ya kutangazwa kuwa isiyo na ugonjwa wa ebola kulingana na taratibu za shirika la afya duniani WHO.
Zaidi ya watu 4000 wameaga dunia nchini Liberia kutokana na ugonjwa wa ebola.
CHANZO BBC.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni