Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Ijumaa, 27 Machi 2015

EBOLA;RAIA WA S LEONE KUSALIA MAJUMBANI.

Raia wa Sierra Leone waanza kusalia majumbani kwa siku tatu kwa lengo la kukabiliana na ebola 
Mamlaka nchini Sierra Leone imeanza kutekeleza hatua ya kutotoka kwa siku tatu miongoni mwa raia wake itakayosaidia kukabiliana na kuenea kwa mlipuko wa ugonjwa wa ebola.
Takriban watu millioni sita wametakiwa kusalia majumbani mwao kwa kipindi cha siku tatu huku watu wa kujitolea wakitembelea nyumba hadi nyumba kuwasaka watu walio na ishara za ugonjwa huo huku wakiwashauri wengine jinsi ya kuepuka maambukizi.
Visa kadhaa bado vinaendelea kuripotiwa kazkazini na Magharibi mwa Sierra Leone kila wiki.
Mataifa matatu ya Afrika Magharibi yalioathiriwa vibaya na Ebola Sierra Leone,Liberia,Guinea-yameweka lengo la kutokuwa na hata kisa kimoja cha ebola ifikiapo katikati ya mwezi ujao.
CHANZO BBC.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni