Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Jumatano, 25 Machi 2015

MAREKANI KUSHAMBULIA IS MJINI TIKRIT.

Rais wa Iraq Fouad Massoum 
Rais wa Iraq Fouad Massoum ametoa ishara kwamba jeshi la muungano linaloongozwa na Marekani huenda likatekeleza mashambulizi dhidi ya wapiganaji wa Islamic State mjini Tikrit.
Katika kipindi cha siku chache zilizopita, muungano huo ulianza kufanya uchunguzi katika mji huo wa Iraq.
Bwana Massoum ameliambia shirika la habari la Reuters kwamba baada ya kukusanya ripoti za uchunguzi wa ndege,muungano huo utaanza oparesheni za kijeshi.
Hadi kufikia sasa ,Marekani imejiondoa katika jaribio la vikosi vya Kishia vya Iran kuuteka mji wa Tikrit.
Hatahivyo jaribio hilo limefeli huku mamia ya wapiganaji wa ISIS wakisalia katikati ya mji.
Rais wa Iraq hajasema iwapo serikali ilitaka mashambulizi ya angani ya Marekani katika mji wa Tikrit.
CHANZO BBC.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni