Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Ijumaa, 27 Machi 2015

NIERIA; JESHI LAICHUKUA NGOME YA B HARAM.

Jeshi la Nigeria lauteka mji wa Gwoza
Jeshi la Nigeria linasema kuwa limeuchukua mji wa kazkazini mashariki wa Gwoza unaoaminika kuwa ngome kuu ya Boko Haram.
Ni katika eneo hilo ambapo wapiganaji wa Boko Haram walitangaza uongozi wa kiislamu na ni miongoni mwa miji mikuu iliotekwa na kundi hilo katika kipindi cha hivi karibuni.
Tangazo hilo linajri siku moja tu kabla ya uchaguzi mkuu nchini Nigeria unaotarajiwa kuwa na ushindani mkubwa.
Uchaguzi huo uliahirishwa kwa mda wa wiki sita ili kutoa fursa kwa jeshi la muungano wa mataifa kupata mda zaidi wa kukabiliana na Boko Haram.
Rais wa Chad,taifa ambalo ni miongoni mwa yale yaliyo na vikosi vyake amesema kuwa vikosi vya Nigeria havijajizatiti.
CHANZO BBC.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni