Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Ijumaa, 27 Machi 2015

JOHN TERRY AONGEZEWA MKATABA CHELSEA.

Nahodha wa Chelsea John Terry aongezewa mkataba 
Nahodha wa kilabu ya Chelsea John Terry ameongeza mkataba wake katika kilabu hiyo hadi mwisho wa msimu wa mwaka 2015-16.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 34,ambaye mkataba wake wa awali unakamilika mwisho wa msimu huu ameichezea Chelsea mara 550.
Chelsea wanaongoza kwa pointi sita katika jedwali la ligi ya Uingereza wakiwa na mechi moja zaidi ambayo hawajacheza dhidi ya wapinzani wao na mkufunzi Jose Mourinho anasema kuwa kandarasi hiyo ya mwaka mmoja si ya kumpatia asante John Terry bali ni kwa sababu anaendelea kucheza vizuri.
Ni mlinzi wa kiwango cha juu.
Mourinho hivi majuzi alisema kuwa ana hakika kwamba Terry atapewa mkataba mpya,ikiwa ni miongoni mwa sera za kilabu hiyo kuwaongezea kandarasi awchezaji ambao wamepitisha umri wa miaka 30.
CHANZO BBC.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni