Mamilioni ya wapiga kura wakipiga foleni katika kituo cha kupigia kura
Mamilioni ya wapiga kura wamejitokeza leo kuchagua wabunge wapya nchini Israeli.
Uchaguzi huo unaushindani mkali ukilinganishwa na chaguzi za awali nchini Israeli.
Waziri mkuu wa sasa Benjamin Netanyahu, anatafuta muhula wa nne na kufanya kuwa mmojawepo wa viongozi wachache kuwahi kushikilia cheo hicho kwa muda mrefu zaidi.
Kwa mjibu wa kura ya maoni ya uchaguzi mkuu, yaliyotolewa majuzi, Chama cha Likud cha Waziri mkuu Netanyahu kinafuatia kile cha muungamo wa chama cha mrengo wa kati na kushoto.
Wakati huo huo, muungano wa chama cha Zionist, wakiongozwa na Yitzhak Herzog na Tzipi Livni, wameamua kushughulikia maswala ya kijamii na uchumi wa taifa,
maswala yanayowakumba moja kwa moja raia wengi wa Israeli.
Akipiga kura yake katika kituo kimoja mjini Jerusalem, Rais wa Israel, Reuven Rivlin, aliwaomba waisraeli wote kujitokeza kwa wingi kupiga kura
Kutokana na sera hiyo wadadisi hawatarajii kuwa chama chochote kitaibuka na zaidi ya robo ya kura zote katika uchaguzi huu.
CHANZO BBC.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni