Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Alhamisi, 5 Machi 2015

WADAIWA KUSHIRIKIANA NA AL-SHABAAB


 wanajeshi wa ngazi za juu nchini Somalia wanachunguzwa kwa kushirikiana na kundi la wapiganaji wa Alshabaab
Mamlaka nchini Somalia imewakamata wanajeshi wake wa ngazi za juu na kuwatuhumu kwa kushirikiana na wapiganaji wa kundi la Al-shabaab.
Tayari maafisa 12 wanachunguzwa kwa madai ya kuwasaidia wapiganaji hao kushambulia hoteli ya The SYL katika mji mkuu wa Mogadishu mnamo mwezi Januari.
Ujumbe kutoka Uturuki ulikuwa ukiishi katika hoteli hiyo ukisubiri ziara ya rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan.
 
wanajeshi wa umoja wa Afrika nchini Somalia
Watu watatu waliuawa katika shambulizi hilo la bomu.
Jeshi la serikali ya Somali linalosaidiwa na vikosi vya Umoja wa Afrika linajaribu kulishinda kundi la Al-shabaab.
CHANZO BBC

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni