Silaha zilizokusanywa kutoka kwa wapiganaji wa FARC
Rais wa Colombia Juan Manuel Santos
anasema kuwa mazungumzo yenye lengo la kumaliza mapigano kati ya
Serikali na wanamgambo wa FARC yataanza hivi karibuni.
Mazungumzo hayo yanaelezwa kumaliza mzozo wa muda mrefu na wapiganaji hao wa mrengo wa kushoto.Katika ujumbe wa mwaka mpya uliotolewa siku ya jumatano, Santos amesema mchakato wa amani uko katika awamu za mwisho, ambapo Rais huyo amesema ni muhimu sana kwa mustakabali wa vizazi vya sasa na vijavyo.
Maswala yanayotiliwa mkazo ni pamoja na maswala ya haki za waathiriwa na kumaliza mzozo nchini Colombia.
Rais Santos amesema wameanza mchakato wa makubaliano juu ya namna watakavyowezesha wapiganaji kuacha silaha na kuingia katika maisha ya uraia.
CHANZO BBC
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni