Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Jumatano, 14 Januari 2015

SIMBA SCMABINGWA WA KOMBE LA MAPINDUZI


Kikosi cha Mnyama-Simba 
Timu ya Simba Sc imeibuka kidedea kwa kutwaa kombe la mapinduzi kwa mikwaju 4-3 dhidi ya Mtibwa Sugar katika mchezo ulipigwa kwenye dimba la Amaani Visiwani Zanzibar.
Dakika tisini za mchezo za kawaida zilimalizika kwa timu hizi kwenda sululu ya bila kufungana ndipo changamoto ya mikwaju ya penati ikafuata .
Penati za simba zilifugwa na Awadh Juma, Hassan Kessy, Hassan Isihaka na Dan Ssenrukuma wakati ya Shaaban Kisiga iliokolewa na Kipa Said Mohamed.
Penati za Mtibwa Sugar zilifungwa na Ally Lundenga, Shaaban Nditi na Ramadhan Kichuya huku Ibrahim Rajab ikigonga mwamba huku penati ya Vincent Barnabas ikiokolewa na kipa Ivo Mapunda.
Nahodha wa Simba, Hassan Isihaka,alikabidhiwa Kombe la Mapinduzi pamoja na Shilingi Milioni 10 kutoka kwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dokta Ali Mohammed Shein.
Kipa Said Mohammed wa Mtibwa Sugar amekuwa kipa bora wa michuano,beki wa kati wa Mtibwa Sugar, Salim Mbonde ameibuka kuwa mchezaji bora wa michuano.Mfungaji bora amekuwa Simon Msuva wa Yanga ambaye alifunga mabao manne.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni