Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Alhamisi, 15 Januari 2015

ISRAELI INATUPELELEZA;HEZBOLLAH


wapiganaji wa kundi la Hebollah
Kiongozi wa kundi la wapiganaji wa Kilebanoni la Hezbollah amethibitisha taarifa zinazodai kuwepo mmoja wa viongozi wa juu ndani ya kundi hilo anatuhumiwa kutumwa na Israel kuwapepeleza.
Shekh Sheikh Hassan Nasrallah amesema kiongozi huyo anayetuhumiwa tayari anashikiliwa na kundi hilo tangu abainike miezi mitano wakati akifanya kazi kwenye idara ya usalama ya kundi hilo la Hezbollah.
Kauli ya Shekh Nasrallah imekuja siku chache baada ya kutolewa taarifa kupitia vyombo vya habari vya Lebanon zinazodai kuwepoa kwa ofisa wa ngazi za juu wa Israel miongoni mwa wapiganaji haoa ambaye yupo kwa kazi maalum.
Hii si mara ya kwanza kwa kundi la wapiganaji wa Hezbollah kujikuta wakiwa na watu wanaowapeleleza miongoni mwao
Hata hivyo Hezbollah imewahi tena kumbaini mtu aliyekuwa akiwapeleleza,japo kuwa kwa sasa usaliti huo unawakumba wakiwa katika wakati mgumu wa mapigano dhidi ya serikali ya Rais Assad.
CHANZO BBC

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni