Kumbu kumbu ya MH17
Kumefanyika maadhimisho ya
kuwakumbuka watu walipoteza uhai wao kwenye ndege ya shirika la ndege
la Malaysia MH17, nchini Uholanzi,ambapo maua na mishumaa ipatayo mia
mbili na tisini na nane vilinavyo wakilisha idadi ya abiria waliokuwa
wakisafiri na ndege hiyo kabla ya ajali ambavyo viliwekwa na
wanafunzi,ndege hiyo ilipopotelea Mashariki mwa Ukraine yapata miezi
minne iliyopita.
Mfalme na malkia wa Uholanzi na mabalozi wa nje
waliomo nchini humo walihudhuria hafla hiyo,ambapo majina ya walikufa
katika ajali hiyo yalitajwa.Ikiwa imetimia miezi minne leo, sababu za ajali hiyo mpaka sasa hazijajulikana,ingawa kikundi cha kigaidi cha Urusi kinashukiwa kuidungua ndege hiyo,ambayo ilikuwa ikifanya safari zake kutoka uwanja wa ndege wa Amsterdam kuelekea Kuala Lumpur Malaysia.
inasemekana ndege hiyo ilidunguliwa kwa kombora, na mara moja serikali mjini Moscow imekanusha taarifa hizo.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni