Binti aliyetendwa na mpenzi wake aliyempenda sana.
Leo tutajifunza kwa undani sifa kumi za mpenzi bora ili tuweze kuwatambua wapenzi wetu kabla ya kuwapa mioyo na utu wetu .
1. Mpenzi wa kweli ni yule ambaye hatangoja kujua nini unahitaji yaani hana sababu ya kusubiri kuombwa ndiyo atoe msaada.Kwa kuwa ana mapenzi ya dhati na anajua mahitaji yako , hawezi kusubiri kushurutishwa au ionekane kama vile anatoa hongo . Kipengele hiki kinawahusu wanaume zaidi .
2. Ni yule atakayejua wakati gani huna furaha au una furaha na atakuwa na wewe kwa hali zote mbili .Hata kama ukiwa huna furaha , hujiona mwenye jukumu kuhakikisha unakuwa nayo kwa namna yoyote ile .
3. Ni yule atayekuwa tayari kukusikiliza kwa kile utakachosema, hatajali umezungumza baya au zuri . Kwa bahati nzuri ni kwamba , ikiwa umekosea , yeye atachukua jukumu la kukuweka sawa.
Asiye na penzi la dhati, ukikosea kwake ni kichekesho . Badala ya kukurekebisha na kukuweka kwenye mstari, atakucheka .
4. Atakuwa na wewe wakati wa shida na raha . Hatakuwa mtu wa kuviziavizia na kujisogeza wakati ukiwa na raha . Kwake, shida yako itakuwa yake akiwa na imani kuwa , hata yake ni yako pia. Anayejiweka kando ukiwa na matatizo , siyo sahihi, mwepuke .
5. Mpenzi wa kweli atakuheshimu na hatapenda kuwa kikwazo cha maisha yako , atakulinda daima.Heshima ni msingi mkuu.
6. Atakupenda kwa moyo wake wote na wala si kwa ajili ya shinikizo fulani . Pesa si kipaumbele chake.
7. Mpenzi wa kweli ni yule atakayeonyesha kuthamini nafasi yako kama rafiki au mpenzi mbele ya wengine , hafichi hisia zake mbele za watu , atakutetea na kukufanya wa kwanza .
8. Kwenye ukweli mpenzi mzuri atasema bila kukuficha na atapenda kukuonyesha mifano ya namna ya kuwa mkweli na mwaminifu.
9. Mpenzi wa kweli ni yule anayejiamini , asiyeyumba katika maamuzi hata kama atalazimika kufanya
maamuzi magumu. Kikubwa ni kusimamia katika ukweli na masilahi yanayoeleweka .
10. Atakuwa tayari kuvumilia , hatakuwa mwepesi wa hasira wala kutumia lugha chafu na ubabe . Nimwelekezaji zaidi , hawezi kukurushia maneno ya kuudhi maana anajua kukuudhi aukukuumiza ni kuharibu maana nzima ya penzi lenu
MC.RAY
WhatsAPP 0659/375263Face booke Raymond Mushi
Page Rashughuli
Histagram MC.RAYMONDMUSHI.
Kijana aliyetendwa na mpenzi wake aliyempenda sana.

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni