Wafanyakazi wa afya huko Sierra Leone
Serikali ya Sierra Leone imesema
italipa dola elfu tano za kimarekani kama fidia kwa familia ya kila
mfanyakazi wa afya ambaye amefariki baada ya kuambukizwa Ebola wakati
akihudumia wagonjwa wa Ebola.
Kituo cha taifa cha kupambana na
Ebola nchini humo kimesema fidia hiyo ya mara moja pia kwa ndugu wa
wafanyakazi wa afya zaidi mia moja ambao wamekufa kwa ugonjwa huo hapo
awali.Virusi vya ugonjwa huo vimekuwa vikisambaa kwa kasi nchini Sierra Leone ambapo katika muda wa siku tatu zilizopita zaidi ya watu mia tatu wamegundulika kuambukizwa ugonjwa huo.
Mwezi uliopita serikali ya Guinea nayo ilisema ingeanza kulipa dola elfu kumi kwa kila familia ya mfanyakazi wa afya aliyeambukizwa Ebola wakati akitekeleza majukumu yake.
chanzo.BBC.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni