Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Jumatatu, 10 Novemba 2014

MAPIGANO MAPYA YAZUKA SUDANI KUSINI

 
Vita vimekuwa vikiendeleea nchini Sudan kwa miezi 11 sasa huku maelfu wakiachwa bila makao

Mapigano mapya yamezuka katika majimbo matatu nchini Sudani kusini , siku chache baada ya pande mbili hasimu kukubaliana kumaliza mzozo ambao umekuwepo kwa miezi 11.
Wiki iliyopita, Raisi wa Salva Kiir na Kiongozi wa waasi Riek Machar walikubaliana kumaliza mapigano kufuatia mazungumzo ya siku mbili nchini Ethiopia.
Serikali na Waasi wamekuwa wakinyoosheana kidole kuwa wamekuwa wakitekeleza mashambulizi katika jimbo la Upper Nile,Unity na Jonglei.
Msemaji wa Waasi Brigedia Jenerali Lul Ruai Koang ameishutumu Serikali kwa kuanzisha mashambulizi dhidi yao hasa katika maeneo yenye mafuta katika jimbo la Unity.
Lakini msemaji wa Jeshi Philip Aguer amesema vikosi vya waasi ndivyo vilivyoanzisha mapigano, kisha wao haraka wakajibu mashambulizi.
Mazungumzo yanayoratibiwa na jumuia ya IGAD,ambayo imetoa muda wa siku 15 kwa pande zote mbili kufikia makubaliano kumaliza mzozo.IGAD imetishia kuweka vikwazo ikiwemo marufuku ya kusafiri na usafirishaji wa silaha,ikiwa makubaliano hayatafikiwa kwa kipindi kilichotolewa.
Maelfu ya Watu wameuawa kwenye mapigano ya Sudani kusini na wengine milioni 1.8 wamekimbia mapigano tangu yalipoanza nchini humo katikati ya mwezi Desemba mwaka jana.
CHANZO, BBC

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni