Kura ya maoni Catalonia
Matokeo ya kura ya maoni isiyokuwa
na makubaliano iliyopigwa jana kutaka ama kutotaka jimbo la Catalonia
lililoko kaskazini mashariki mwa Hispania kutaka kujitenga yanaonesha
zaidi ya asilimia themanini ya wapiga kura wamepigia kura kujitenga kwa
eneo hilo, huku kukiwa tayari asilimia tisini ya kura zimehesabiwa.
Kura
hiyo ya maoni imelenga kutathmini idadi ya watu wanaotaka Catalonia
kuwa nchi huru.Mapema kiongozi wa Catalonia Artur Mas ameelezea zoezi
hilo la upigaji kura kama ni mafanikio.Hata hivyo serikali ya Hispania imesema kura hiyo ni ya bure na haiathiri chochote.Waziri wa Sheria wa nchi Rafael Catala hiyo amesema zoezi hilo halikuwa la kidempokrasia na kulielezea kama lisilo na mafanikio yoyote na lisilofaa.
Zoezi hilo la upigaji kura limefanyika baada ya mahakama ya katiba nchini Hispania kuamuru kufanyika kwa kura hiyo ya maoni.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni