Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Jumapili, 9 Novemba 2014

MATOKEO YA AWALI CATALONIA

Kura ya maoni Catalonia
Matokeo ya kura ya maoni isiyokuwa na makubaliano iliyopigwa jana kutaka ama kutotaka jimbo la Catalonia lililoko kaskazini mashariki mwa Hispania kutaka kujitenga yanaonesha zaidi ya asilimia themanini ya wapiga kura wamepigia kura kujitenga kwa eneo hilo, huku kukiwa tayari asilimia tisini ya kura zimehesabiwa.
Kura hiyo ya maoni imelenga kutathmini idadi ya watu wanaotaka Catalonia kuwa nchi huru.Mapema kiongozi wa Catalonia Artur Mas ameelezea zoezi hilo la upigaji kura kama ni mafanikio.
Hata hivyo serikali ya Hispania imesema kura hiyo ni ya bure na haiathiri chochote.Waziri wa Sheria wa nchi Rafael Catala hiyo amesema zoezi hilo halikuwa la kidempokrasia na kulielezea kama lisilo na mafanikio yoyote na lisilofaa.
Zoezi hilo la upigaji kura limefanyika baada ya mahakama ya katiba nchini Hispania kuamuru kufanyika kwa kura hiyo ya maoni.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni