Huduma za benki nchini Somalia
Serikali ya Somalia imesema kuwa
uamuzi wa benki moja nchini Marekani kufunga akaunti za kampuni za
kuhamisha fedha nchini Somalia utaathiri usalama ulioafikiwa nchini
humo.
Benki ya Merchants kutoka jimbo la Carlifornia,ambayo
husimamia asilimia 80 ya fedha zote zinazoelekea nchini Somalia, imesema
kuwa inaondoa huduma zake nchini humo kutokana na madai ya mapya ya
biashara ya fedha chafu.Mwakilishi wa umoja wa mataifa nchini Somalia Nicholas Kay ,amesema kuwa hatua hiyo inaleta wasiwasi mkubwa kwa kuwa usafirishaji huo wa fedha ndio mfumo wa maisha ya raia wa Somalia.
Raia wa Somalia nchini Marekani hutuma nyumbani zaidi ya dola millioni 200 kila mwaka.
CHANZO BBC
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni