Maandalizi ya dawa ya ebola nchini Liberia
Kwa upande mwingine madaktari na
maafisa wa afya wanakutana mjini London Ijumaa kujadili ni mambo gani ya
kuzingatiwa kutokana na mlipuko wa ugonjwa wa Ebola katika mataifa ya
Afrika Magharibi.
Wajumbe watakuwa wanaangalia uharaka wa
kimataifa katika kukabiliana na mlipuko na namna uduni wa miundombinu ya
sekta ya afya katika nchi za Guinea, Liberia na Sierra Leone
ilivyosababisha kuenea kwa ugonjwa huu. Wataalam pia watakuwa
wanchunguza namna ambavyo dawa mpya za tiba na chanjo ya ugonjwa wa
Ebola zinavyofanya kazi.Alhamisi shirika la utafiti wa tiba la Ufaransa limesema matokeo ya dawa mpya dhidi ya ebola ambazo zinafanyiwa majaribio nchini Guinea zimeonyesha matokeo ya kutia moyo katika kupambana na ugonjwa huo.
CHANZO BBC
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni