Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Jumatatu, 9 Februari 2015

MAREKANI ITAPELEKA SILAHA UKRAINE.


Rais Barack Obama na Angela Markel
Rais wa Marekani Barack Obama amesema kuwa Marekani inatafakari kupeleka silaha nchini Ukraine kusaidia kukabiliana na Waasi wanaoiunga mkono Urusi.
Akizungumza katika Ikulu ya White House baada ya mazungumzo na Kansela wa Ujerumani Angela Markel, Obama amesema nia itakuwa kuisaidia Ukraine kuimarisha ulinzi kuliko kulishinda jeshi la Urusi. Lakini amesema ana matumaini kuwa suluhu ya kidiplomasia itapatikana.
“Ubabe wa Urusi umeimarisha umoja wa Marekani na Ujerumani na washirika wetu duniani kote na ningependa kumshukuru Angela kwa uongozi wake imara na ushirika wetu tunapokutana na changamoto hii.Tunaendelea kusisitiza kupatikana kwa suluhu kwa njia ya diplomasia”amesema Obama
Naye Kansela wa Ujerumani Angela Markel haoni kama njia za kijeshi zinaweza kuumaliza mzozo huu.
chanzobbc

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni