Raia wa Jordan waandamana kupinga islamic state
Maelfu ya riaa wa Jordan
wameandamana katika mji mkuu , Amman, wakiunga mkono serikali yao katika
vita inavyotekeleza dhidi ya kundi la Islamic State baada ya kumuua
rubani wa ndege za vita wa Jordan.
Serikali ya Jordan inasema kuwa
ndege zake za vita zilifanya mashambulizi kadhaa ya angani zikilenga
wapiganaji wa Islamic State huko Syria Alhamisi.Maafisa wa usalama wa Jordan wanaarifiwa kuwa ndio waliokuwa wakilengwa na mashambulizi huko Raqqa, eneo lenya ufuasi mkubwa wa IS nchini Syria.
Hadi sasa mataifa manee ya kiarabu yakijumuisha Jordan yanahusika katika kampeni kali inayoongozwa na Marekani dhidi ya Islamic state kupitia mashambulizi ya angani.
CHANZO BBC
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni