kiongozi wa burkina faso isaac Zida
Rais wa Ghana,Nigeria na Senegal
wanatarajiwa kuwasili nchini Burkina Faso hii leo kwa ajili ya kutoa
msukumo kwa Jeshi la nchi hiyo lirudishe utawala wa kiraia.
Kiongozi
wa mpito Luteni Kanali Isaac Zida amesema jeshi litaachia madaraka
ndani ya majuma mawili,muda uliopangwa na Umoja wa Afrika.Zida ameahidi kuanzisha serikali ya Umoja ili kuepuka vikwazo ambavyo vinaweza kutolewa dhidi yao.
Jeshi lilichukua madaraka baada ya kutokea machafuko na maandamano yaliyoshinikiza kujiuzulu kwa Rais Blaise Compaore.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni