Shule

Shule
Shule ya secondary Lilasia yenye usajili no. 3878 inatoa nafasi za kujiunga na kidato cha 1 mwaka 2015 shule ni ya kutwa na bweni. ofa! lipia kwa awamu nne. mawasiliano:- 0754 504 132/ 0756 240 471/ 0754 985 772 Wahi sasa nafasi ni chache

Ijumaa, 6 Februari 2015

JORDAN YAAPA KUIMALIZA IS KWA KILA HALI.


Mfalme Abdullah wa Jordan aahidi kupambana na Waasi wa Islamic State
Jordan imesema mashambulizi ya anga dhidi ya Wanamgambo wa Islamic State ni mwanzo tu wa kulipa kisasi kwa tukio la kumteka nyara Rubani wa nchini humo, Waziri wa mambo ya nje wa Jordan,Nasser Judeh ameeleza.
Judeh ameiambia CNN kuwa Jordan inafanya kila jitihada kupambana na IS.
Awali Jordan ililenga maficho ya wanamgambo nchini Syria, lakini Judeh amesema Operesheni zao zimefika mpaka Iraq.
kauli hii imekuja baada ya Wanamgambo wa IS kuonyesha Video waliokuwa wakimchoma moto Rubani Moaz al-Kasasbeh akiwa hai.
Baada ya shambulio la siku ya Alhamisi,Ndege za kivita zilikwenda mpaka katika Kijiji cha Rubani huyo, ambapo Mfalme wa Jordan Abdullah wa pili alienda kuonana na Familia ya Marehemu.
CHANZO BBC

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni